Tuesday, February 13, 2007

UBEPARI & other kids stuff

Huyu jamaa kanifikirisha sana, anasema kwa kipindi tunachoiishi sasa duniani kuna maendeleo ya tekenolojia kuliko vipindi vyote lakini ikitakiwa kifanyike kitu kimoja cha maana kama kulisha watu walio katika shida inakuwa... mmhh
Anasema jamaa wa magharibi hawana maji kukatika, watoto wanakwenda shule ,kuna kujisika salama lakini je wanajisikia vizuri?
Anasema ubepari ni kama gari bovu ambalo viongozi wanalitengeneza lakini halitengemai wewe unalipia lakini gari lako halitengemai...
Anasema yeye hataki mchango wako bali anataka wewe ujiulize maswali ya hali ya mambo duniani....
Anatoa mfano wa jinsi watoto wakiwa wanacheza huwa wanagombana lakini hupatana baada ya muda mchache lakini hawa watoto ukumbuke hawajajifunza diplomasia yausuluhishi wala nini...inakuwaje huu utaratibu unavyokuja kuharibika na maana yake nini nini?...
Na mambo kadha wa kadha.
Basi msikilize huyu jamaa (anaelezea kwa muda mrefu kidogo hivyo inabidi uwe na muda wa kumsikiliza) ,fuata maelezo yake kwa kumsililiza moja kwa moja kupitia viungo alivyoweka nenda pale anapokuwambia watch online . Huyu jamaa anapatikana hapa. Mimi nakubaliana nae kwa mambo mengi tu aliyoyasema.