Friday, September 29, 2006

ELIMU GANI?

Katika pita pita kwangu kwenye blogu (huu mjadala wa neno hili kwa kiswahili sijui uliishia wapi) nili kutana na bwana Charahani kichwa cha Habari Tutaosha miguu ya bodi...? bonyenza hapa na Bwana Mjengwa kichwa cha habari Kama si juhudi zako... bonyeza hapa wakizungumzia swala la Elimu basi nikaona nikiweka maoni kwenye blogu zao maoni yangu yatakuwa marefu sana ni bora niyaandike hapa kwangu. Mabwana hawa wamezungumzia vitu vingi ila mimi nachangia kiujumla kuwa swala halisi hapa ni sio ni kwa jinsi gani elimu inachangia kwa maendeleo ya jamii lakini ni Elimu gani inafaa, kwa maendeleo ya aina gani na kwa faida ya nani? Iwapo tutachambua hili ndio tutajua nini kinafanyika kwa sasa hivi na nini chakurekebisha. Unaweza kukuta kuwa linatengenezwa tabaka la watumishi na watumikiwa au vinginevyo kwa jinsi elimu inavyofadhiliwa na kusambazwa kuna uwezekano mkubwa wa kujenga uwiano usio sawa wa kimapato na unajua kinachofuata. Lakini ili kujua hilo lazima tujadili hilo swali letu. Huu utaratibu wa kusema somo hili linafaa na hili halifai nao unatokana na mtazomo wa kusema elimu ni nini? Huu ndio mjadala unaotakiwa.

katika historia watu wamekuwa wakikumbana na ukweli wa mabadiliko yanayowazunguka . Ni rahisi kuona mabadiliko ya muda mfupi yanayoonekana kila siku yanayotuzunguka lakini vigumu kungamua mabadiliko makubwa yanayotokea kwa muda mrefu. kwa mfano wanahistoria wanafikiria kwamba himaya ya Roma ilikufa kwa wakati mmoja katika historia (kila mmoja anatoa sababu yake kuwa ilivyovamiwa na Alaric 410 a.d au kwa kuondoloewa kwa mfalme wa mwisho wa roma 476 ad n.k) lakini kuhusu wenyeji wa Roma waliona vipi haya matukio? Je walijua kuwa baadae hawa wanahistoria watawaeleza kwa ajabu sana kukua na kufa kwa himaya yao? Kwa wao hawakuona kuanguka kwa himaya yao ( kwa karne 3 kati ya miaka ya Marcus Arelius na na kuzidiwa kwa Roma na Barbarians(sijui kiswahili chake ingawa neno hili nalo lina utata wa kihistoria katika lugha hiyo) karne ya 15 A.D. kipindi hiki kilijulikana kama kukua na kufa kwa himaya ya Roma). kwa wao biashara ya himaya yao iliendelea kama kawaida, wafanya biashara waliendelea kuisha kama watawala,matajiri waliendela kuvaa nguo zao za kifahari na maaskari waliendela kupigana na barbarians hata kama ilikuwa ni kwa pesa na sio kwa kulinda Roma. Hivyo hawakufanya kitu ili kulinda himaya yao na ndio kitakachotokea kwetu iwapo hatushtuka. Nitaendelea siku nyingine nimepatwa na mgeni wa ghafla...

Monday, September 25, 2006

TAASISI YA MASOMO YA AFRIKA?

Ni mara nyingi nimeona na kusikia kila chuo kikuu kina Taasisi ya Masomo ya maendeleo,au Taasisi ya Masomo Ya Afrika. Iwe chuo hiko kiko Afrika au Ulaya au Marekani au Asia. Hizi Taasisi zina jishugulisha na kusoma mambo ya Afrika kuanzia Historia,lugha,Uchumi,siasa na kadha wa kadha. Lakini cha kushangaza ni kuwa sijawahi kusikia wala kuona katika vyuo vyetu vikuu vya Tanzania au (Afrika) Hapa nigesisitiza Tanzania, maana kidogo naufahamu zaidi nayo. Kuwa tuna Taasisi ya Masomo ya Ulaya/Marekani/Asia. Hivi ni kweli sisi hatuitaji kuwasoma hawa jamaa au tunasubiri wao ndio watuambie tuwasome nini, mbona wao wanatusoma kwa faida gani? Hebu hawa wasomi wanaosema kwamba katika majadiliano na hawa mabwana kwenye meza tukikaa nao tunakuwa na ufahamu mmoja je ni ya kweli haya? Kwanini sisi hatuna?