Wednesday, November 08, 2006

NGUVU ZA SODA AU.......?

Najuwa wengi tunaufahamu huu msemo wa nguvu za soda.. yaani unaona tumbo limejaa kwa muda baadae ile gesi kutoka unasikia du kumbe hamna kitu tumboni. Basi ndio nadhani wengi ambao mmekuwa mnanitembelea hapa mnaona mbona hamna kipya Ndabuli ameandika au zilikuwa nguvu za soda? La hasha ila nilitingwa na jukumu la ....sijui ni kweli... la kufuta ujinga au kujijaza ujinga..nikaona ngoja ni kaepembeni kidogo, wale walimu waliobobea kwenye vyuo vikuu kuna wakati wanachukua likizo waiita sabbatical(sijui kwa kiswahili) nikaona ngoja na mimi nijipe hiyo lakini wapi nikaona nina kitu...wanasema ni ka ugonjwa ... yaani ni teja la kompyuta! Kila nikikaa karibu yake nikisema niandike mambo mengine basi vidole vinaniwashwasha inabidi kuanza kuangalia blogu mbalimbali,lakini si yangu, (si ni ya kwangu najua nini kilichomo)...aah lakini kumbe watu wanaacha maoni.
Basi nikakuta Bwana Kitururu kaacha swali. Bwana Kitururu swali lako nalijibu kuwa kaa mkao wa kula ile Habari nitaimalizia. Kama wahenga walivyosema ahadi ni deni basi hilo deni nitalilipa. Nikakutana tena na Bwana Ngurumo ananipa heko zake na kunipiga na swali. Bwana Ngurumo nimependa swali lako na majibu yangu ni kuwa nimependa kujipa jina moja kwani ni rahisi kwa watu kulikumbuka hilo jina na jina hilo halitoi picha au mtazamo wa muelekeo wowote ambao utamfanya mtu kutotaka kusoma (au kusoma ..mmh sijui?) blogu yangu. Jina hili pia lina historia yake ambayo inahusiana na kupenda kwangu kuuliza hivi inakuwaje? Napenda pia umoja huu wa jina kwani mtu atatoa maoni yake bila kushawishiwa na jina. Ila mtu akipenda kuwasiliana nami zaidi anaweza kutumia anuani yangu ya barua pepe.Ila Bwana Ngurumo usiwe na shaka sikuziendavyo tutatambulishana.
Basi kwa kumalizia nitajitahidi sasa kuandika mambo yanayonikuna na mambo haya ni mengi,sitabobea katika swala moja tu, ni lolote litakalo nikuna ..mbona yapo mengi, elimu, siasa, historia,vichekesho..na hata habari za kupaka rangi ya bluu ya anga(sky blue) kwenye choo kwani rangi hii nasikia inzi hawaipendi (sijui ni kweli?...nalifanyia utafiti) na kadha wa kadha.
Ila nakuomba endelea kunitembelea.