Si Kawaida yangu kuanza kaundika jambo linalonikera ghafla lakini hili nimeshindwa kuvumilia. Nilipata kukutana malumbano kati ya Chahali na watu wa Globalpublishers wa Tanzania.
Katika malumbano yao niliona bwana Chahali akiwa na hoja nyingi zenye msingi katika hilo swala waliliokuwa wakibishania(kwa upande wangu). Ingawaje nilikuwa msomaji tu lakini maoni yao wote yalikaa kichwani mwangu.
Kilichotokea sasa ni ijumaa moja ya gazeti linalochapishwa na globalpublishers lilitoa picha ambayo ilileta utata (hasa kwangu mimi) na wengine kuhusu uwezo wa watoa habari hawa kwani hizo picha nilipata kuziona kitambo sehemu nyingine. Kilichonishtusha ni kuwa zilitumiwa kama ni habari mpya iliyotokea huko nyumbani. Baada ya kusoma hizo habari nilisema kweli sasa tumekwisha...yaani hawa wachapishaji wanafanya kitu kama hiki? Nikamkumbuka Chahali ni kasema hapa hana tena la kujitetea ni kuacha mwenye macho atazame. (Chahali nakuunga mkono aslimia 200! kwa magazeti ya Udaku). Kweli kwenye uongo ukweli ujitenga.
Nashukukuru kwa watu wengi kuwatolea macho hadi wao wamefuatilia hilo swala na kulifanyia kazi soma hapa na hapa.
Inatia aibu sana na ndio maana nilaandika kuwa ni vizuri mara nyingi kujiuliza Hadithi hiyo kakufundisha nani?

4 comments:
Blessings:
Today is my birthday and I thought I'd ask people to please visit and share with 2 friends, that we may end this 'Conspiracy of Silence' regarding the TRUTH behind the Human Rights Abuses that occur daily, with impunity, in Canada & the world.
your humble servant,
ancient clown
Hadithi hiyo kakufundisha nani?:-)
Swali linaniua sana hilo! LoL!
Hadithi nyingine siku hizi, nikijifanya nimeitunga, rahisi kustukiwa nadanganya.
Nachukia internet kwa ujumla, Google na viutaalamu fulani vya kutafuta vingine, visasababishavyo twaweza kustukiwa kirahisi kuwa kuna kasoro fulani kwenye hadithi.
Samahani, natoka nje ya somo!
Njoo tumalizie kujadili kipengele, ili tuende kwenye hatua nyingine ya kuboresha wanajumuiya wa jumuiya ya Watanzania wanao tembelea au wanao blogi.
Tembelea hapa : http://blogutanzania.blogspot.com/
ilia tumalize kujazia dondoo ili tu anze na kipengele kingine.
Idumu JUMUWATA!
Salama Mkuu?
Post a Comment