Monday, September 25, 2006

TAASISI YA MASOMO YA AFRIKA?

Ni mara nyingi nimeona na kusikia kila chuo kikuu kina Taasisi ya Masomo ya maendeleo,au Taasisi ya Masomo Ya Afrika. Iwe chuo hiko kiko Afrika au Ulaya au Marekani au Asia. Hizi Taasisi zina jishugulisha na kusoma mambo ya Afrika kuanzia Historia,lugha,Uchumi,siasa na kadha wa kadha. Lakini cha kushangaza ni kuwa sijawahi kusikia wala kuona katika vyuo vyetu vikuu vya Tanzania au (Afrika) Hapa nigesisitiza Tanzania, maana kidogo naufahamu zaidi nayo. Kuwa tuna Taasisi ya Masomo ya Ulaya/Marekani/Asia. Hivi ni kweli sisi hatuitaji kuwasoma hawa jamaa au tunasubiri wao ndio watuambie tuwasome nini, mbona wao wanatusoma kwa faida gani? Hebu hawa wasomi wanaosema kwamba katika majadiliano na hawa mabwana kwenye meza tukikaa nao tunakuwa na ufahamu mmoja je ni ya kweli haya? Kwanini sisi hatuna?

1 comment:

Anonymous said...

I yhink you need to make your website more intresting and add some languages for people who do not speak kiswahili.