Wednesday, February 07, 2007

HADITHI HII KAKUFUNDISHA NANI?

Nadhani ni wengi wanakumbuka msemo huu... umehadithiiaaa weee,.. umemaliza hadithi yako..au..hapana umesiikiliza wee hadithi hadi imekwisha... halafu yule shangazi anakuuliza hadithi hii kakufundisha nani? .... maana yake ni nini? Majibu si mnayakumbuka.
Ngonja ni kupe kisa kimoja kilinitokea wakati huo nikiwa Sekondari. Sekondari ile (sikutajii mpaka unipe mji!...aa wapi huo unanonipa sitaki) naikumbuka kwa sheria zake ,
1.Yaani tulikuwa haturuhusiwi kuchomekea mashati, basi si unajua utukutu wa shule yaani sheria zote unapingana nazo, basi watu walikuwa wanachomekea, ukimuona mwalimu wa nidhamu(alikuwa anaitwa jina la utani Kicheche) au ukiitwa ofisini ndio unachomoa shati(hapo palikuwa patamu hapo hebu jifikirishe mwenyewe!),
2. Shule zote zilikuwa na Lebo/nembo kwenye shati lakini sisi hatukuwa na nembo..na
3...aah ngoja niishie hapo... turudi kwenye kwenye kisa.
Kipindi kile kilikuwa cha mbio za mweng,e basi mwenge ulikuwa unapita pale shuleni. Yule kiongozi wa mwenge kama tujuavyo anakuwa na ujumbe wa mwenge,basi akatoa ule ujumbe wa mwenge(hatasikumbuki ulikuwa nini?) Basi yule jamaa alipomaliza kwa sababu tulikuwa kimya mwanafunzi mmoja aliuwahi ule ukimya akamuuliza yule ndugu AAGH! yule kiongozi wa mwenge. (tena kwa sauti KUUBWAA) HADITHI HIYO KAKUFUNDISHA NANI?.... Basi nakwambia yule kiongozi wa mwenge alibaki mdomo wazi... na shule nzima ilipasuka kicheko. Kilichofuata mwenye unajua...(si adhabu)
Lengo langu la kukuambia kisa hiki ni kukumbusha kuwa kuna maswala mengi ambayo kwa njia moja ama nyingine ni vizuri mtu kuuliza hadithi hii kakufundisha nani?mfano.. Unaposoma kitabu, Gazeti, jarida, unaposikiliza hotuba za watawala,au majibu au utaratibu si vibaya kuuliza haditihi hhi kakufundisha nani au kamfundisha nani au Kuuliza alikwambia maana yake nini? Sio lazima uulize kwa sauti jaribu kujiuliza mwenye ili upate jibu litakalo kufaa. Kuna mambo mengi ambayo tumekuwa tukiyakubali bila kujua maana yake ni nini.
Nitaendelea Kukuletea mifano ya kujiuuliza ..... (ila usiniliuze sasa na wewe hadithi hii kanifundisha nani.teh..tehe..tehe) Baadae.