Thursday, March 15, 2007

YALIYONIVUTIA MTANDAONI

Leo sina cha kuandika (aa mbona naandika lakini...!) Ninacho cha kuandika, katika pilikapilika zangu za kufanya mkono uende kinywani nimesahau kile kijiti changu (memory stick) cha kuhifadhi kumbukumbu ambacho mara nyingi huwa nakitumia kuhifadhi maandishi yangu mengi, na jamaa mmoja ambaye amenifahamisha anacho, muda wa kuonana nae kwa leo hana basi lengo nililokuwa nataka kufanya leo limeshindikana nikasema lakini nina muda wa kuaandika mawili matatu hapa, basi leo ninaandika yaliyonivutia katika pitapita zangu mtandaoni.
Ngoja nianze na "Blooks prize" vitabu 15, kutoka nchi tano tofauti vimetajawa ambavyo vitashiriki katika kuchaguliwa kupata zawadi ya lulu. Blooks ni vitabu ambavyo vinatokana na blogu, yaani yale mambo yako uliyoyaandika unayafanya kitabu. Mshindi wa mwaka jana alikuwa aliyekuwa na blogu amabayo aliandika MWAKA WANGU WA KUPIKA VIBAYA/HATARI (MY YEAR OF COOKING DANGEROUSLY) na inasemekana ameuza kopi 100,000 na inategemewa sinema kutengenezwa.
Wakenya nao wamenifurahisha na hii tovuti yao ya mzalendo waone hapa Hii ilianza baada ya wabunge wakenya kujipandishia mishahara mwaka 2003..lakini watu walikuwa hawajui nini hasa wafanyacho basi wakaanzisha mzalendo ambapo wanaandika kuhusu kila mswaada upitao bungeni, kila hotuba na kila mbunge aliye katika bunge wasome hapa

Lingine ni lile sakata la bomba la mafuta kwenda kanda ya ziwa ambapo mkataba wa dollar 2.6 billion umepatiwa Kampuni za Kigeni unaolalamikiwa na wazawa wanaosema wamenyanganywa tenda limechukua sura mpya baada ya Kuonekana kuwa Chama cha Mapinduzi kina mkono wake hapo kupitia kampuni ya chama iitwayo Tanzania Green company Limited soma zaidi kuhusu sakata hilo hapa.
Heee......Alamsiki.. (jamaa mwenye kijiti changu anasema kapata muda mchache wa kuonana na mimi ngoja nimuwahi..!)