Friday, October 13, 2006

UTAMKIKE KIRAHISI!...NA NANI?

Wiki hii ni wiki ambayo kutakuwa kumbukumbu ya kifo cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Ni kumbukumbu ya kufikisha miaka saba tangu alipofariki dunia. Alifariki oktoba 14,1999. Langu mimi si kuzungumzia hizi kumbukumbu...sasa unataka kuzngumzia nini?
Nachotaka kuzungumzia ni kitu kingine kabisa ila kimeanzia kwenye Jina la Nyerere. Ni muda si mrefu ule uwanja wetu tunaoita wa kimataifa wa ndege Dar es salaam, ulibadilishwa jina na kuitwa Mwalimu Julius K. Nyerere International Airport. ...Sasa?..
Lakini sasa nimesikia kuwa eti wameondoa "mwalimu" na "K" ili utajike vizuri,.... ama!!! Utajike vizuri na nani sasa? Hapo kweli nimeshindwa kuelewa kuwa hawa watoa majina wanamtazamo gani? Kwani ni watanzania na wanaoongea kiswahili wangapi wanashindwa kutaja mwalimu! au K! Navyo fikiri mimi hata hilo jina lilivyobadilishwa lilikuwa halijatambuliwa sehemu nyingi ...kivipi?...
Umeisha wahi kujaribu kuangalia au kununua tiketi ya ndege katika mtandao,au kuangalia bei zake,au ratiba kwa safari zianziazo Dar es salaam au Kuishia hapo. Kwa kutumia huo utaratibu mashirika mengi ya ndege na makampuni wakala wa usafiri huwa wakionyesha sehemu uendapo na jina la kiwanja cha ndege lakini mpaka hvi karibuni sijaona ukitambuliwa kama mwalimu K. Nyerere....Sawa.. sasa wewe unachotaka kusema ni nini?
Lakini hili la kubadilisha ili litamkike nimeshindwa kulielewa kama ni kwa ajili ya nani? Kama ni kwa wageni wasiojua Kiswahili, kwanini wasijiufunze kutamaka hilo? sisi ndio tuwabadilishie kwa fadia ipi? Na wao mbona hata kubadilisha kutambua kuwa sio tena Dar es salaam international airport hawajafanya hivyo. Unajua airport moja Thailand inaitwaje? Suvarnabhumi International, Taiwani? unaitwa Taiwan Taoyuan International Airport , na mingine mingi tu inamajina kwa lugha yao. ..Kwa hivyo?... Ni wangapi unaowajua wewe wanaweza kutamka hayo majina? Umeishasikia watu hawataki kutumia uwanja kwasababu hawawezi kuutamka?.....MMMH.
Na kumbuka nimekutana na jamaa wengi wasio watanzania na katika kutambulishana nikisema mimi ni mtanzania utasikia oohh mwalimu nyerere!..... but what does mwalimu mean because I think it is not his really name? Basi inabidi kueeleza. Utasikia.... ooh thats interesting...
Mbona hawajabadilisha The mwalimu nyerere foundation iwe The Nyerere foundation. Hiyo foundation haitakiwi kutamkika? Tena nadhani hiyo ndio watu wantakiwa kuitaja sana maana NADHANI inatoa misaada.
Huu ndio mimi naona ni utumwa wa mawazo. Kwanini tusiendeleze kile tulichonacho? Ndio maana hata Raisi mstaafu wa msumbiji alituaibisha kwa yeye kuongea kiswahili wakati sio lugha rasmi katika nchi yake. Yeye akiwa mstari wa mbele kupigia chapuo lugha hii lakini wenyewe wenye kusema ndio lugha rasmi tuko kimya.Hili jambo linanifikirisha sana je ni utumwa wa akili au ni kutokujua?

Sunday, October 08, 2006

WARUSI MHH..NINA WASIWASI!

Jumamosi ya tarehe 7 oktoba 2006 nimesoma na kusikia kuwa mwandishi mmoja wa habari wa urusi Anna Politkovskaya ameuwawa kwa kupigwa risasi bonyeza hapa kusoma inasemekana mwandishi huyu wa habari alikuwa mstari wa mbele katika kuandika habari za ukiukaji wa haki za binadamu unaofanywa na serikali ya Urusi. Na ni wiki hiyohiyo ambapo kulikuwa na mtafaruku kati ya serikali ya Urusi na Georgia uliosababisha Urusi kuwarudisha nyumbani wa georgia kibao kwao bonyeza hapa kusoma. Haya matukio hasa hili la kuwarudisha wageorgia limenifanya nikumbuke unyama ambao warusi wanawafanyia wageni hususan wanaotokea Afrika au weusi (Peter Tosh mwanamuziki wa miondoko ya reggae aliimba mwimbo mmoja unaosema as long as you are blackman you are an African,no matter where you are coming from,Bonyeza hapa usome beti za wimbo huo. Haijali unatokea wapi,iwapo wewe ni mweusi ni mwafrika) Huko Urusi hasa mji wa st.petersburgh watu weusi wamekuwa wakiuwawa kwa wingi na bila ya watu kupiga makelele kama yanayopigwa sasa bonya hapa kusoma. Sipingi watu kupiga Kelele ila naona kelele zenyewe zinapigwa kwa kuangalia rangi. Najua kuwa sehemu nyingi duniani hali ndivyo hivyo ilivyo lakini, Juzijuzi raisi Urusi alifanya safari ya Afrika (kuna mwanablogu mmoja au Habri mmoja sikumbuki nilisoma wapi waliipa jina habari hiyo the scramble for Africa) na hakuna sehemu niliyosikia kuwa hili jambo likizungumzwa. Ndio maana nasema Urusi... mmhh. Hasa kwa wale wanaopata scholarship za Kwenda huko.