Wednesday, September 20, 2006

Daruso Hata Tovuti?

Katika kusoma soma kwa magazeti ya nyumbani katika mtandao ili angalau nijue kinachoendelea nimesoma kuna mgogoro Mkubwa sana kati ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam na Bodi ya mikopo. Jambo moja nililoliona ni ubishi wa gharama za maisha chuoni. Basi katika kutafakari mgogoro huu mawazo yangu yalinipeleka mbali sana. Nikajiuliza hivi Daruso ina tovuti yake? Hilo jambo sijaliona sasa najiuliza hivi hawa wasomi wetu wameshindwa kweli kutengeneza tovuti?Nikajisemea Hawa Daruso hawana tovuti, lakini wana miradi wanaendesha kwani hii miradi inawasaidia katika nini? Nimeona mifano ya vyama vya wanafunzi katika vyuo vikuu nchi nyingine vikiwa na uwezo wa kufungua migahawa yao ambayo inaendeshwa kwa bei za kiuanafunzi. kwanini wanafunzi wasijijenge kiuchumi ilikuondokana na Tatizo kama hili. Nielewavyo mimi hiki chama kipo kisheria na siku moja katika blogu ya bwana michuzi niliona picha moja ikionyesha jinsi eneo la chuo kikuu likiwa linaota majengo ya vitega uchumi, nikajiuliza hawa Daruso nao wananyanyua kitega uchumi chao ili kuondokana na huu mnyanaso nikasema sidhani kama tovuti hawana itakuwa ili wazo. Je, kweli tutaweza kujisadia wenyewe?