Monday, April 23, 2007

Nimerudi tena Jamani. Baada ya kufuta vumbi nyumbani na kusalimia mtaani nikaona ngoja niwabeep (au niwa dipu kama anavyosema Chesi Mpilipili) wale walionitembelea wakati sipo na kuacha ujumbe na wale waliopita kimyakimya. Katika mihangaiko yangu nilifika pale Parisi, Ufaransa na nilitembelea ule mnara wao maharufu (ingawa walitaka kuuondoa mwanzoni) wa Eiffel. Kilichonifurahisha pale Kileleni niliona wameonyesha ni umbali gani uliopo kutoka Hapo Kileleni hadi Mwanza na Dar es salaam.
Angalia pale juu kileleni ndio kuna hayo maandishi hapa chini



Huu ni umbali Kutoka Kileleni mwa mnara wa Eiffel Kuelekea Mwanza.



Na huu ni umbali Kuelekea Dar es salaam.