Wednesday, June 13, 2007

NIKO NYUMBANI (yaani niko Tanzania)

Jamani, kimya hiki kisiwatishe sana kwa sasa niko Tanzania, nakata mikoa na ndio maana sionekani huku.
Ni kitambo nilikuwa sijatemebelea nyumbani basi muda mwingi unatumika katika kusalimia ndugu, jamaa na marafiki pamoja na kudodosa mambo kadha wa kadha ambayo nayaona.
Tatizo moja ni kuwa muda mwingi ndio huo natumua kucatchup na jamaa na kuonja zile larger!!! .. muda wa kukaa na kuandika kidogo haupo na vilevile si niko likizo jamani...(au kublog hakuna likizo?)..mmmh na mitandao huku mingi iko taratibu (basi muda wa kwenda kwenye kikao unapungua) sana sana nasomea kwenye simu yangu ila kuandika ndio ...hapa.. basi natarajia nikitulia nitaendelea kutoa nikifikiriacho..
Karibu tena

1 comment: